Wednesday 13 January 2016


  • Andaa kitunguu, nyanya, pilipili hoho na karoti. Osha, kata vipande vidogo tayari kwa mapishi.
  • Andaa tui la nazi – vunja nazi, kuna na kisha kamua tui zito na hifadhi vizuri pembeni.
  • Weka sufuria ya kupikia jikoni, kisha mimina mafuta ya kula kiasi. Subiria yapate moto vizuri.Weka vitunguu kwenye sufuria.
  • Koroga mpaka vianze kubadilika rangi kidogo.
  • Vitunguu vikianza kubadilika rangi, weka dagaa wa double T. Koroga na kukaanga vizuri dagaa wa double T kwa muda wa dakika chache.Dagaa wa double T wakianza kukauka 
  • kamulia ndimu au limao juu yake. Koroga kiasi kisha weka pilipili hoho na karoti. Endelea kukoroga.
  • Weka nyanya kwenye dagaa. Endelea kukoroga na kisha funika na mfuniko ili nyanya ziive vizuri na mvuke na kuwa laini.
  • Nyanya zikiiva unaweza kuziponda ili kupata rojo nzuri...pia unaweza kuongeza tomato paste kama nyanya chache au mbichi...
  • Weka chumvi unayoona inafaa kutokana na kiwango cha mboga.

0 comments:

Post a Comment

Whasapp tunapatikana kwa 0687599999 au piga simu 0714584583 www.instagram.com/doubletfood