Wednesday, January 13, 2016
- Andaa kitunguu, nyanya, pilipili hoho na karoti. Osha, kata vipande vidogo tayari kwa mapishi.
- Andaa tui la nazi – vunja nazi, kuna na kisha kamua tui zito na hifadhi vizuri pembeni.
- Weka sufuria ya kupikia jikoni, kisha mimina mafuta ya kula kiasi. Subiria yapate moto vizuri.Weka vitunguu kwenye sufuria.
- Koroga mpaka vianze kubadilika rangi kidogo.
- Vitunguu vikianza kubadilika rangi, weka dagaa wa double T. Koroga na kukaanga vizuri dagaa wa double T kwa muda wa dakika chache.Dagaa wa double T wakianza kukauka
- kamulia ndimu au limao juu yake. Koroga kiasi kisha weka pilipili hoho na karoti. Endelea kukoroga.
- Weka nyanya kwenye dagaa. Endelea kukoroga na kisha funika na mfuniko ili nyanya ziive vizuri na mvuke na kuwa laini.
- Nyanya zikiiva unaweza kuziponda ili kupata rojo nzuri...pia unaweza kuongeza tomato paste kama nyanya chache au mbichi...
- Weka chumvi unayoona inafaa kutokana na kiwango cha mboga.
0 comments:
Post a Comment
Whasapp tunapatikana kwa 0687599999 au piga simu 0714584583 www.instagram.com/doubletfood